Klabu ya Gor Mahia ya Kenya imepata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Petro Atletico ya Angola katika uwanja wake wa nyumbani wa Kasarani mjini Nairobi. Gor Mahia ikiwa na wachezaji tisa tu uwanjani baada ya wachezaji wake wawili kulimwa kadi nyekundu na kocha wao Hassan Oktay, klabu hiyo imefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya shirikisho barani Afrika katika mchezo huo wa mwisho wa hatua ya makundi.
Gor Mahia sasa inaungana na Nkana ya Zambia, Etole du Sahel, CS Sfaxien zote kutoka Tunisia, RS Berkane, Hassania Agadir kutoka Morocco, Zamalek ya Misri na Al-Hilal ya Sudan.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |