Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang leo amesema China itatoa msaada kwa Msumbiji, Malawi na Zimbabwe ambazo zimekumbwa na kimbunga Idai.
Bw. Geng Shuang amesema, China iko tayari kutoa msaada kadri inavyoweza, kuendana na hali ya maafa na mahitaji ya serikali za nchi hizo tatu.
Kimbuga Idai kimesababisha vifo vya watu 84 nchini Msumbuji, 56 nchini Malawi na 98 nchini Zimbabwe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |