Mchezo wa mwisho wa kundi L kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka huu kati ya wenyeji timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itakapoikaribisha timu ya taifa ya Uganda (Uganda Cranes) jumapili wikiendi hii uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam utachezeshwa na marefa kutoka nchini Gabon.
Eric Otogo Costane mwamuzi wa kati, atasaidiwa na washika vibendera Moussounda Montel na Marlaise Ditsoga Boris ambapo mchezo huo utapigwa majira ya saa 1:00 usiku
Tayari wachezaji wote wa kulipwa wa Tanzania wameshawasili na kuanza mazoezi na wenzao jana jioni. Uganda Cranes imepiga kambi nchini Misri kujiandaa na mchezo huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |