• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri mkuu wa China ahimiza juhudi ili kutimiza lengo la mwaka

    (GMT+08:00) 2019-03-21 09:28:07

    Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang amehimiza juhudi ili kutimiza lengo la mwaka na kazi mbalimbali zilizowekwa kwa mwaka huu.

    Bw. Li amesema hayo katika mkutano wa baraza la serikali, huku akiongeza kuwa idara za serikali zinatakiwa kuchukua hatua halisi haraka iwezekanavyo kumaliza kazi muhimu ambayo ni pamoja na kuimarisha mageuzi na ufunguaji mlango, kurahisisha utaratibu wa kisiasa, na kupunguza ushuru na ada.

    Mkutano huo ulioongozwa na waziri mkuu umesisitiza utekelezaji wa sera na mipango ya kazi iliyowekwa, na kutoa wito kwa utoaji wa fedha kuunga mkono sera hizo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako