Rais Xi Jinping wa China amekutana na mkuu wa Chuo Kikuu cha Harvard Bw. Lawrence Bacow hapa mjini Beijing na kueleza matumaini yake kuwa mawasiliano ya kitamaduni kati ya China na Marekani, yanaweza kuwa na matokeo mazuri zaidi. Rais Xi amesema ushirikiano wa kielimu unasaidia kuongeza ufahamu wa umma juu ya urafiki wa pande mbili, na China inahimiza kufundishana na kuwahamasisha wanafunzi wa China kusoma nje, na kuunga mkono mawasiliano na ushirikiano wa kielimu na nchi nyingine. Hii ni mara ya kwanza kwa Bw. Bacow kufanya ziara nje ya nchi tangu ashike wadhifa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |