Afisa mkuu wa mikakati katika Benki ya Standard Chartered kitengo cha kusimamia mali Steve Brice amesema viwango vya juu vya riba katika soko la Marekani na dola iliyoimarika vimeendelea kupungua.
Kutokana na hilo, dhamana zinazotolewa na mataifa kama Kenya huvutia bei nzuri.
Amesema hali hiyo itafanya dhamana ya Kenya kuwa na ushindani sokoni, hivyo bei itavutia zaidi kuliko ilivyokuwa.
Kenya inataka mkopo kutoka Eurobond kama moja ya kufadhili upungufu wa bajeti wa Sh635.5 bilioni. Kati ya hizo, Sh321.5 bilioni zinatarajiwa kupatikana kutoka soko la nje.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |