Rais Hassan Rouhani wa Iran ameeleza kusikitishwa kwake na hatua ya rais Donald Trump wa Marekani kukubali kwa upande wake kipekee madai ya Israeli kuwa milima ya Golan ni sehemu ya nchi hiyo.
Televisheni ya Iran imemnukuu rais Rouhani akisema kuwa, si rahisi kufikiri kwamba Marekani inaweza kuipa nchi nyingine eneo la nchi moja kwa kukiuka sheria na kanuni za kimataifa.
Rais Rouhani ameongeza kuwa, kuimarisha ushirikiano kati ya nchi na kanda ni njia muhimu katika kupambana na Marekani na Israeli.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |