Chelsea walipewa adhabu ya kutofanya usajili wa mchezaji yoyote baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kina na kudaiwa kuwa walimsajili staa wa Burkina Faso Bertrand Traore akiwa na miaka 16 mwaka 2017, kitu ambacho ni kinyume na sheria na kanuni za FIFA.
Baada ya kukata rufaa ya kupinga hukumu hiyo, FIFA imepanga kusikiliza shauri la Chelsea Aprili 11 ili kutoa uamuzi wa mwisho, adhabu waliyopewa Chelsea iliambatana na faini ya pound 460,000 huku FA pia wakipigwa faini ya pound 390,000.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |