Katika taarifa yake, IAAF imesema wakimbiaji 582 kutoka mataifa 67 watashuka mjini Aarhus kuwania ubingwa hapo Machi 30.
Wanariadha 557 kutoka mataifa 60 walishiriki makala ya mwaka jana jijini Kampala nchini Uganda.
Zaidi ya wakimbiaji 300 wamejiandikisha kutimka katika vitengo vya watu wazima, huku wanariadha 200 walio chini ya umri wa miaka 20 pia watashiriki mashindano hayo mjini Aarhus katika kilomita nane kwa wanaume na kilomita sita kwa wanawake.
Vile vile kuna mchezo wa kupokezana vijiti ambapo kutakuwa na vikosi vya timu zinazojumuisha wanaume na wanawake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |