Benki ya Equity imesmea inatafuta fursa za kuwekeza nchini Ethiopia ikiwa ni sehemu ya mpango wake wa kuwa benki ya bara la Afrika.
Mkurungezi mkuu wa benki hiyo James Mwangi amesema kwa sasa Equity ina mtaji wa dola bilioni 1.3 na imeanza upya mipango yake ya upanuzi barani Afrika.
Mwangi alisema benki hiyo inafuatilia sera za mageuzi nchini Ethiopia na iko kwenye mipango ya kuanza oparesheni nchini humo.
Ethiopia ina benki 18 za kibiashara huku serikali ikimiliki Commercial Bank of Ethiopia na benki ya Maendeleo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |