Maduka ya uchumi nchini Kenya kwa mara nyingine tena yamekosa kuwasilisha ripoti ya fedha ya kipindi kilichokamilika mwezi Juni mwaka 2018 licha ya kuongezewa muda wa ziada wa miezi mitano kufanya hivyo.
Pia Uchumi imekosa kutoa ripoti yake ya kipindi cha nusu mwaka cha hadi disemba 2018.
Mamlaka ya soko la mitaji CMA inazitaka kampuni zote kwenye soko la hisa la Nairobi kuchapisha ripoti zake za kifedha.
Mwkaa uliopita Uchumi ilisema wakaguzi wake wa hesabu wataanza kazi mwezi Januari mwaka huu na kutoa ripoti mwishoni mwa mwezi machi lakini bado hawajafanya hivyo au kutoa taarifa yoyote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |