Baraza la Katiba nchini Algeria limethibitisha kujiuzulu kwa rais Abdelaziz Bouteflika na litaliarifu bunge baadaye siku ya kuwa wazi kwa nafasi ya rais kwa mujibu wa Kifungu namba 102 cha Katiba. Spika wa Baraza la Juu la Bunge Bw. Abdelkader Bensalah atashika nafasi ya mkuu wa taifa kwa siku 90, ambapo uchaguzi wa rais unatakiwa kufanyika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |