Serikali ya Uganda itaanza kutumia Mfumo wa Manunuzi wa Kielekroniki mwezi Julai mwaka huu katika idara zake kumi kabla ya kuueneza kwenye idara zote za serikali mapema mwaka kesho.
Maneja Manunuzi ya Kielektroniki wa Mamlaka ya Manunuzi ya Umma na Usimamizi wa Mali za Umma PPDAA Florence Nakyeyune, amesema hatua hiyo inalenga kudhibiti ufisadi na ucheleweshaji katika manunuzi ya umma.
Kwa mujibu wa wizara ya fedha, Mfumo wa Manunuzi wa Kielekroniki utapunguza gharama ya kufanya manunuzi kwa asilimia 30, na bajeti ya manunuzi ya mwaka inachukua asilimia 20 hadi 30 ya Pato la ndani la taifa GDP.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |