• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri mkuu wa Uingereza ataka EU kuahirisha muda wa Brexit mpaka tarehe 30 Juni

    (GMT+08:00) 2019-04-05 19:33:28

    Waziri mkuu wa Uingereza Bibi Theresa May jana ameuomba Umoja wa Ulaya kuahirisha muda wa Brexit mpaka tarehe 30 Juni.

    Bibi Theresa May ameandikia barua kwa mwenyekiti wa kamati ya Ulaya Donald Tusk akisema, Uingereza inapendekeza kuwa muda wa Brexit uishe tarehe 30 Juni mwaka huu, na kama pande mbalimbali zinaweza kuridhia kabla ya tarehe hiyo, muda huo utakamilika kabla ya tarehe hiyo.

    Bibi May amesema, serikali ya Uingereza inapenda kukubali mpango huo, ambao unakubali Uingereza kujiondoka kutoka Umoja wa Ulaya kabla ya tarehe 23 Mei, lakini serikali itaendelea kuwajibika na maandalizi kwa ajili ya uchaguzi katika tarehe hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako