Kasi ya Mkenya huyo ni dakika moja na sekunde 35 bora kuliko rekodi ya awali ya saa 2:23:47 ambayo Muitaliano Maura Viceconte amekuwa akishikilia tangu mwaka 2000.
Kwa upande wa wanaume, Vincent Kipchumba wa Kenya amerejesha nchini Kenya taji la Vienna, imemchukua saa 2:06:56 kuibuka mshindi mbele ya Mswizi Tadesse Abraham aliyetumia saa 2:07:24 na mganda Solomon Mutai aliyemaliza kwa kutumia saa 2:08:25. Zaidi ya wanariadha 41, 000 kutoka mataifa 110 walishiriki makala hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |