• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Mfumko wa bei wapaa Tanzania

    (GMT+08:00) 2019-04-09 17:08:59
    Mfumko wa bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia Machi 2019 umeongezeka hadi asilimia 3.1 kutoka 3.0 kwa mwaka ulioishia Februari 2019.

    Hali hiyo imetokana na bidhaa zisizo za vyakula kama vile mavazi na viatu, kodi ya pango, mafuta ya taa, mkaa, kuni, huduma za afya zimechangia kuongezeka kwa mfumuko huo.

    Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephrahim Kwesigabo, alisema hali hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Machi mwaka huu, imeongezeka kidogo ikilinganishwa na Februari.

    Alisema kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa Taifa kumechangiwa hasa na kuongezeka kwa bei za baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi cha mwaka ulioishia Machi mwaka huu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako