Hamilton alishinda licha ya kuwa nyuma ya madereva wa Ferrari kwa kipindi kirefu cha mbio hizo. Kwanza Sebastian Vettel alikabiliwa na shinikizo na gari lake lilipoteza muelekeo. Kisha mambo yakawa mabaya hata zaidi kwa Ferrari baada ya injini ya gari la kiongozi wa mbio hizo Charles Leclerc kuanza kupoteza umeme.
Leclerc alimaliza katika nafasi ya nne nyuma ya Valtteri Bottas wa Mercedes wakati timu hiyo ikishinda nafasi mbili za kwanza katika mbio mbili za msimu huu.
Max Verstappen wa timu ya Red Bull alimaliza wa nne huku Mjerujamani Vettel akinyakua nafasi ya tano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |