• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Ligi ya mabingwa Ulaya- Mambo ni hatari fire- Man U wapoteza nyumbani, Juventus na Ajax hakuna mbabe

    (GMT+08:00) 2019-04-11 08:49:37
    Baada ya kusubiriwa kwa hamu kwa zaidi ya wiki mbili na mashabiki wa soka, hatimae usiku wa jana katika uwanja wa Old Trafford ulichezwa mchezo wa Manchester United dhidi ya FC Barcelona, huo ukiwa ni mchezo wa kwanza wa robo fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya unaojulikana zaidi kama UEFA Champions League msimu wa 2018/2019.

    Barcelona wameendeleza ubabe baada ya kumpiga Man United kwa goli 1-0 lilipatikana kwa Luke Shaw kujifunga baada ya Luis Suarez kupiga kichwa alichopigiwa krosi na Lionel Messi dakika ya 12 ya mchezo,

    Man United kama wanataka kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo watalazimika kwenda Nou Camp wiki ijayo kupata ushindi wa kuanzia magoli 2-0, au 2-1 na kuendelea.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako