Mkutano wa 140 wa Umoja wa Mabunge Duniani, IPU uliomalizika jana mjini Doha umetoa taarifa ya mwenyekiti ukilaani Marekani kwa kutambua mamlaka ya Israel katika Milima ya Golan nchini Syria. Taarifa hiyo imesema kitendo cha kuchukua kwa mabavu ardhi ya nchi nyingine kwa njia ya vita hakikubaliki, na hatua ya Marekani imekiuka maazimio husika ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na italeta ugumu mkubwa zaidi katika kutimiza haki na amani ya kudumu katika Mashariki ya Kati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |