• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yatumia dola za Kimarekani milioni 18.8 kukabiliana na ukame

    (GMT+08:00) 2019-04-11 09:52:28
    Kenya imetumia dola za Kimarekani milioni 18.8 kukabiliana na athari za ukame nchini humo ambao umewaathiri watu takriban milioni 1.1.

    Waziri wa ugatuzi nchini humo Eugene Wamalwa amesema, ingawa wataalam wameona mvua haitanyesha kwa wakati, lakini serikali imeandaa fedha kusaidia kukabiliana na janga hilo.

    Bw. Wamalwa pia amesema, serikali imetoa dola za Kimarekani milioni 6 kununua magunia elfu 26,200 ya mahindi, elfu 17,060 ya maharagwe na elfu 15,420 ya mchele ambavyo tayari vimeshatolewa kwa wahitaji, na dola nyingine milioni 6.8 za Kimarekani zimepelekwa kwenye idara ya maji kwa ajili ya kusafirisha maji na kukarabati visima.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako