Tanzania imethibitisha kutokea kwa mlipuko kwa homa ya Dengue mjini Dar es salaam, na kusema watu 252 wameripotiwa kuambukizwa.
Naibu waziri wa afya Bw. Faustine Ndungulile amethibitisha kuwa mlipuko pia umeripotiwa mkoani Tanga, ambako watu 55 wamethibitishwa kuambukizwa. Akiongea na wanahabari mjini Dodoma, Naibu waziri Bw. Ndungulile amesema mamlaka za afya zinaendelea kufuatilia ugonjwa huo katika nchi nzima.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |