• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mbio za kupokezana za Ukanda Mmoja na Njia Moja zazinduliwa nchini Tanzania

    (GMT+08:00) 2019-04-15 09:10:05

    Benki ya Standard Chartered nchini Tanzania jana imezindua mbio za kupokezana za Ukanda Mmoja na Njia Moja, ambazo ni za kwanza za kimataifa kuandaliwa na Benki hiyo katika mazingira ya pendekezo la Ukanda Mmoja na Njia Moja lililotolewa na China.

    Uzinduzi wa mbio hizo mjini Dar es Salaam umeifanya Tanzania iwe nchi mwenyeji wa 31 wa mbizo za Ukanda Mmoja na Njia Moja, ambazo zimezinduliwa na bolazi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke.

    Mbio hizo zimeongozwa na wafanyakazi wanane wa benki ya Standard Chartered, ambao walichaguliwa kutoka matawi ya benki hiyo kutoka Asia, Afrika, Mashariki ya kati, Ulaya na Amerika.

    Wachezaji hao wanatarajiwa kushirki kwenye mbio hizo katika masoko 44 ya Ukanda Mmoja na Njia Moja ndani ya siku 90.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako