Ligi kuu Tanzania Bara imeendelea jana, katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, Coastal Union waliwakaribisha Wekundu wa Msimbazi Simba ya Dar es Salaam. Hadi mwisho wa mchezo Simba imeondoka na pointi 3 kwa kufunga magoli 2-1. Magoli ya Simba yamefungwa na Meddie Kagere.
Mchezo mwingine ulikuwa mjini Morogoro kati ya wakata miwa wa Turiani Mtibwa Sugar walipowaadhibu Yanga ya Dar es Salaam kwa goli 1-0.
Yanga bado wanaongoza ligi hiyo ikiwa na alama 74, ikifuatiwa na Azam FC yenye alama 66 huku Simba yenyewe iko nafasi ya tatu kwa alama 60 lakini hadi sasa imeshacheza michezo 23.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |