Mashindano ya Pikipiki: Uganda yaitambia Kenya kibabe, yabeba ubingwa
(GMT+08:00) 2019-04-24 08:26:03
Mashindano ya ubingwa wa kuendesha pikipiki Afrika Mashariki na kati yamefanyika katika uwanja wa Busiika nchini Uganda, na kushuhudiwa Mganda Maxime Pevan akiibuka bingwa baada ya kukusanya alama 1,395 huku mkenya akiambulia alama 252 tu.
Maxime sasa anajiandaa kwa mashindano ya Afrika yatakayofanyika mwezi Agosti mwaka huu nchini Uganda.