Rais Xi Jinping wa China amesema, China itachukua hatua kadhaa muhimu za mageuzi na kufungua mlango, na kuimarisha mipango ya sera na muundo, ili kufungua mlango zaidi kwa nje.
Hatua hizo ni pamoja na kuongeza sekta zinazoruhusu uwekezaji wa nje, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kulinda hakimiliki za kiubunifu, kuongeza ununuzi wa bidhaa kutoka nchi za nje, kufanya uratibu wa kimataifa wa sera za kiuchumi kwa ufanisi zaidi, na kutilia maanani zaidi utekelezaji wa sera za kufungua mlango.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |