Rais Xi Jinping wa China leo amesema, China itaimarisha uratibu wa sera ya jumla na makundi mbalimbali ya uchumi duniani, ili kuhimiza kwa pamoja uchumi wa dunia uwe na nguvu ya kuongezeka, uwe na maendeleo endelevu na kuendelea kwa uwiano.
Rais Xi amesema, China haitashusha thamani ya fedha zake ili kujilinda kibiashara, itakamilisha siku hadi siku utaratibu wa ubadilishaji wa fedha za Renminbi, kulifanya soko lifanye kazi ya kuamua ugawaji wa raslimali, kudumisha utulivu wa kimsingi wa ubadilishaji wa fedha za Renminbi kwenye kiwango cha halali na uwiano, na kuhimiza utulivu wa uchumi wa dunia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |