Maonyesho ya kimataifa ya kilimo cha maua ya mwaka 2019 yamefunguliwa leo hapa Beijing, ambapo rais Xi Jinping amehutubia ufunguzi wa maonyesho hayo.
Viongozi na wajumbe maalumu kutoka nchi 11, wakurugenzi wa mashirika ya kimataifa, wadau wa viwanda na biashara, wataalamu maalumu wa kilimo cha maua wapatao 900 wamehudhuria ufunguzi wa maonyesho hayo. Kabla ya kuhudhuria ufunguzi, rais Xi Jinping wa China na viongozi wa nchi mbalimbali walitembelea jumba la China la maonyesho hayo.
Maonyesho hayo yatafanyika kwa muda wa siku 162, na nchi na mashirika ya kimataifa 110 yatashiriki kwenye maonyesho hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |