• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa kwanza wa Kazakhstan Nursultan Nazarbayev apewa tuzo ya urafiki ya China

    (GMT+08:00) 2019-04-28 21:01:21

    Tarehe 28 mchana, rais Xi Jinping wa China amekutana na rais wa kwanza wa Kazakhstan Nursultan Nazarbayev, ambapo rais Nazarbayev alimwambia rais Xi Jinping kwamba hii ni mara ya 19 kwa kukutana kwangu na rafiki wangu Xi, atatunza daima urafki kati yake na rais Xi.

    Bw. Nazarbayev mwenye umri wa miaka 79 alijiuzulu mwezi uliopita. Mara hii, alikuja China kuhudhuria mkutano wa pili wa baraza la wakuu la ushirikiano wa kimataifa la "Ukanda Mmoja, Njia Moja" akiwa ni rais wa kwanza wa Kazakhstan.

    Leo rais Xi ametoa tuzo ya ngazi ya juu ya urafiki ya China kwa Bw. Nazarbayev. Na kusema kuwa, rais Nazarbayev ni mwanasiasa mwenye ushawishi mubwa wa kimataifa, pia ni mwanzishi na msukuma wa uhusiano wa kiwenzi na kimkakati wa pande zote kati ya China na Kazakhstan.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako