Wakati huo huo, watoto wa darajani Stamford Chelsea the blues imetoka sare ya 1-1 na Eintacht Franfurt baada ya kiungo wake Pedro kuipatia timu yake bao la ugenini. Franfurt ilianza kupata bao kupitia mshambuliaji Luka Jovic ambaye alipata pasi nzuri kutoka kwa Filip Kostic.
Sare hiyo inamaanisha kwamba Chelsea itakuwa timu ya kwanza kucheza mechi 16 za Europa League bila kushindwa, Arsenal wao sasa itaelekea Valencia kwa awamu ya pili siku ya Alhamisi ya wiki ijayo wakitumai kuzuia kushindwa kwa nusu fainali yao ya pili baada ya kuondolewa na Ateltico madrid mwaka uliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |