Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China CPC na Baraza la Serikali la China limetangaza miongozo ya kuhimiza maendeleo shirikishi ya miji na vijiji. China imepata maendeleo makubwa katika kuhimiza upanuzi wa miji na kuleta uwiano katika maendeleo kati ya sehemu za mijini na vijijini tangu mkutano mkuu wa 18 wa CPC. Miongozo hiyo inalenga kuondoa vizuizi vya maendeleo kati ya miji na vijiji ili kuhimiza ustawi wa vijiji na kuongeza kasi ya maendeleo ya kilimo cha kisasa na maeneo ya vijijini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |