Baada ya Jumapili kupata uongozi mpya, klabu ya Yanga ya Dar es Salaam chini ya mwenyekiti mpya Dkt. Mshindo Msolla ambaye aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), amewataka wanachama wa klabu hiyo sasa kuvunja makundi na kuwa kitu kimoja.
Msolla amesema kuna kila sababu ya kuvunja kambi hizo na kuungana pamoja kuijenga klabu hiyo ambayo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikiendeshwa kwa kuungaunga.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |