Kocha wa Arsenal Unai Emery amewataka wachezaji wake kuelekeza akili, macho yao na kuwa makini katika ligi ya Ulaya, baada ya kuona mambo yanakuwa magumu katika ligi kuu ya Uingereza inayoelekea ukingoni.
Arsenal wanapigiwa upatu kukutana na Chelsea katika fainali ya ligi hiyo ya Ulaya baada ya kuwachabanga Valencia goli 3-1 mchezo wa kwanza wa nusu fainali uliopigwa wiki iliyopita. Wakati Chelsea wamejipa uhakika wa kushiriki michuano ya klabu bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |