Kampuni ya teknolojia ya China Huawei imesema kwenye taarifa kuwa ina imani kuwa mhasibu wake mkuu Bi. Meng Wanzhou hana hatia. Meng alikamatwa mjini Vancouver, Canada mwezi Disemba mwaka jana kufuatia ombi la Marekani la kumpelekea huko. Taarifa hiyo imetolewa baada ya kesi ya Meng kusikiliziwa mahakamani jana huko Vancouver. Imesema amri ya kukamatwa kwake iliyotolewa na Marekani ni kinyume na sheria na inatokana na madhumini ya kisiasa badala ya sheria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |