Shirika la hilali nyekundu nchini Kuwait limetangaza kutoa chakula kwa watu wenye mahitaji katika nchi 15 za Afrika, Asia, Ulaya na Mashariki ya Kati kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhani. Mwenyekiti wa shirika hilo Bw. Hilal Al-Sayer amesema shirika lake litatoa chakula kwa watu wapatao laki moja katika nchi mbalimbali zikiwemo Mauritania, Uganda, Kenya, Palestina, Pakistan, Sri Lanka, Yemen na Iraq, pamoja na wakimbizi wa Syria walioko nchini Jordan na Lebanon.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |