Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Palestina UNRWA limesema zaidi ya nusu ya watu wa ukanda wa Gaza watakabiliwa na uhaba wa chakula ifikapo mwezi Juni. Taarifa iliyotolewa na shirika hilo imesema uwezo wake wa kuendelea kutoa misaada kwa wakimbizi milioni moja wa Palestina kwenye ukanda wa Gaza utakabiliwa na changamoto kubwa, kama halitapata fedha za ziada za dola milioni 60 za kimarekani kabla ya Juni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |