Kaimu Katibu mkuu wa kamati ya Olimpiki ya Kenya Francis Mutuku amewaambia waandishi wa habari kuwa maafisa hao leo jumanne watakutana na Meya wa mji wa Yokohama na baadaye watatembelea kiwanja kipya cha mpira wa wavu. Kenya na Japan zilisaini ushirikiano ambao utawezesha timu ya Olimpiki ya Kenya kupiga kambi katika kisiwa cha Kyushu jimbo la Fukuoka kujiandaa kwa mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika Tokyo Japan mwakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |