Kundi la Houthi nchini Yemen limetangaza kuwa chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa, operesheni ya kipindi cha kwanza ya kuondoa vikosi vyake kutoka mji wa bandari wa Hodeidah imekamilika.
Mtandao wa televisheni wa Masirah unaounga mkono kundi la Houthi umethibitisha kuwa vikosi vya kundi hilo vimeondoka kutoka bandari kuu za mji huo.
Mjumbe wa Houthi wa Tume ya Pamoja ya Uondokaji na Uratibu (RCC), amesema Umoja wa Mataifa utaitaka serikali ya Yemen itimize ahadi yake ya kuondoa majeshi kutoka Hodeidah kama kundi la Houthi lilivyofanya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |