Saudi Arabia imetangaza kuwa vituo vyake viwili vya pampu za mafuta ghafi vimeshambuliwa kwa ndege zisizo na rubani. Waziri wa nishati wa nchi hiyo Bw. Khalid Al-Falih ametaja mashambulizi hayo kama ni vitendo vya kigaidi vinavyolenga uzalishaji wa mafuta, na kusema mashambulizi hayo na mashambulizi dhidi ya meli nne zikiwemo boti mbili za mafuta za Saudi Arabia yaliyotokea Jumapili karibu na bandari ya Fujarirah nchini Umoja wa Falme za Kiarabu UAE yalilenga kuvugura utoaji nishati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |