• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • NDONDI: Baada ya kumpiga Breazeale KO ndani ya sekunde 43, Mbabe Wilder amtumia salamu za vitisho Antony Joshua

    (GMT+08:00) 2019-05-20 09:33:08

    Alfajiri ya kuamkia jana nchini Marekani kulikuwa na pambano la ngumi uzito wa juu la WBC kati ya mbabe Deontay Wilder na Dominic Brazeale, Pambano ambalo Wilder ameibuka kwa ushindi wa KO ndani ya sekunde 44 za raundi ya kwanza.

    Na hivi ndivyo mambo yalivyokuwa, mchezo ulitangazwa na kituo cha Runinga cha Sky Sports cha nchini Marekani

    Baada ya Wilder kumpiga ngumi moja Brazeale na kuanguka chini na kushindwa kuendelea na pambano hilo, hivyo ushindi huo unamfanya Wilder kuendelea kutetea ubingwa wake wa WBC uzito wa juu, ushindi huo wa Wilder unakuwa ni ushindi wake wa 40 wa KO katika mapambano yake 42 aliyocheza.

    Mara baada ya mpambano huo, Wilder amewataja Anthony Joshua pamoja Tyson Furry wapo kwenye mipango yake na atawapitia kama upepo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako