Shirika la habari la Yemen, Saba, linaloongozwa na kundi la Houthi limeripoti kuwa waasi wa kundi hilo wamekanusha ripoti za Saudi Arabia kuwa makombora ya kundi hilo yalirushwa dhidi ya mji wa Mecca. Msemaji wa jeshi la Houthi Yahya Sarea amesema hii si mara ya kwanza kwa Saudi Arabia kuwashutumu kuhusu kushambulia Mecca kwa makombora, na kitendo hicho kinalenga kutafuta uungaji mkono juu ya uvamizi wao wa kijeshi dhidi ya watu wa Yemen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |