Kundi la kiislamu la Hamas limekanusha ripoti zilizotolewa na vyombo vya habari vya Israel kuwa limefikia makubaliano ya kusimamisha vita na Israel katika Ukanda wa Gaza kwa miezi sita. Msemaji wa Hamas katika ukanda huo Fawzi Barhoum amesema makubaliano yoyote kati ya Hamas na Israel yanatakiwa kuwa kwenye msingi wa Israel wa kutekeleza makubaliano yote yaliyofikiwa awali. Wakati huohuo, kiongozi mwandamizi wa Hamas katika Gaza Basim Naeem ameliambia shirika la habari la China Xinhua kuwa hakuna makubaliano yoyote yaliyofikiwa, isipokuwa maelewano ya utulivu yaliyopatanishwa na Misri na Umoja wa Mataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |