Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May amesema Muswada wa Makubaliano ya Brexit utajumuisha upigaji kura kuhusu kama kutafanyika zoezi lingine la upigaji kura ya maoni. Amesema hii itakuwa ni fursa ya mwisho ya kumaliza mchakato wa Brexit, na kama wabunge wakipiga kura kukataa Muswada huo kupitiwa kwa mara ya pili, inamaanisha wamepiga kura ya kusimamisha Brexit. Kauli hiyo mpya ya Theresa May imekuja baada ya mazungumzo ya wiki sita kati ya serikali na chama cha upinzani cha Leba yaliyomalizika wiki iliyopita bila kupata maendeleo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |