Kuendelea kudorora kwa bei na soko la kahawa duniani kumeathiri sana mapato ya taifa la Uganda. Kwa kipindi cha miezi 12 iliyopita, Uganda imepoteza shilingi bilioni 386. Kulingana na ripoti iliyotolewa na Halmashauri ya Ustawishaji wa Kahawa Uganda juma lililopita, mapato ya nje ya kahawa kati ya Aprili 2018 na Aprili mwaka huu 2019, yalishuka hadi dola milioni 418 kutoka dola milioni 521. Ripoti hiyo vile vile inaonyesha kwamba idaid ya kahawa iliyouzwa nje ilipungua kwa asilimia 11.6.