• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Mbappe abeba tuzo mbili Ligue 1 Ufaransa

    (GMT+08:00) 2019-05-23 09:00:00

    Mshambuliaji wa Paris Saint Germain, Kylian Mbappe anayetakiwa na Real Madrid akiwa ameshika tuzo yake ya Mchezaji bora wa mwaka wa ligi ya Ufaransa (Ligue 1) aliyoshinda pamoja na ya Mchezaji Bora Chipukizi baada ya kukabidhiwa jana mjini Paris, Ufaransa.

    Mbappe ambaye amemaliza ligi kwa kufunga jumla ya magoli 30, amekuwa mchezaji wa kwanza mwenye umri mdogo kutwaa tuzo hiyo kwa misimu mitatu. Mwaka 2017 alipewa tuzo baada ya kushinda ligi 1 akiwa na klabu ya Monaco.

    Mchezaji wa zamani wa Ivory Coast na nyota wa Chelsea, Didier Drogba amepata tuzo ya mchango kwa jamii.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako