Shirika la Afya Duniani WHO limethibitisha kuwa Algeria na Argentina zimetokomeza malaria baada ya nchi hizo kutoshuhudia maambukizi ya ugonjwa huo katika miaka mitatu iliyopita. Algeria ni nchi ya pili ya Afrika kutambuliwa na WHO kutokuwa na ugonjwa wa Malaria baada ya Mauritius, iliyothibitishwa mwaka 1973, huku Argentina ikiwa ni nchi ya pili katika bara la Amerika kuthibitishwa katika miaka 45 iliyopita baada ya Paraguay mwezi Juni mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |