• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kiongozi wa Sudan Kusini autaka upinzani kutekeleza kihalisi makubaliano ya amani

    (GMT+08:00) 2019-05-24 09:33:32

    Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amewataka viongozi wote wa upinzani kufanya juhudi halisi katika kutekeleza makubaliano ya amani, ili kurejesha matumaini na matarajio ya wananchi.

    Rais Kiir amesema, baada ya Amani kupatikana, nchi hiyo yenye historia fupi duniani itatimiza maendeleo ya kasi kutokana na utajiri wake wa maliasili.

    Amesema hayo katika uzinduzi wa jengo la wizara ya ulinzi ya Sudan Kusini, na kuongeza kuwa, kwa muda mrefu, maliasili za nchi hiyo zimepotea, ikiwemo rasilimali ya watu katika mapambanno ya wenyewe kwa wenyewe. Amesema kama nchi hiyo ikiendelea kuwa na utulivu wa hivi sasa, nchi hiyo iliyokumbwa na mapambano itatimiza maendeleo mkubwa ya miundombinu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako