Kenya jana imependekeza kuwa mwenyeji wa Sekritarieti ya Eneo la Biashara Huria barani Afrika (AfCFT).
Katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje ya Kenya Bw. Macharia Kamau amewaambia waandishi wa habari huko Nairobi kuwa, sera ya mambo ya nje ya Kenya inalenga kutekeleza ahadi ya maendeleo na usalama wa bara la Afrika kwa kupitia Agenda 2063.
Bw. Kamau amesema kuweka ofisi ya sekretarieti nchini Kenya sio tu kutaimarisha umuhimu wa Kenya kwa kuwa nchi ya uongozi katika biashara na pande nyingi, bali pia kutaletea fursa nzuri kwa bara la Afrika kuendeleza biashara huria na kunufaisha nchi zote barani humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |