Wizara ya Sheria ya Marekani imesema imefungua mashtaka mapya 17 dhidi ya mwanzilishi mwenza wa WikiLeaks Julian Assange, ikiwemo kupokea na kutangaza nyaraka za siri za kijeshi na kidiplomasia mwaka 2010 kinyume cha sheria. Ameshtakiwa kukiuka sheria ya ujasusi ya Marekani. Hata hivyo vyombo mbalimbali vya habari vya Marekani vimesema mashtaka mapya yameyatilia mashaka masuala ya Marekebisho ya Kwanza, ambayo yanaweza kutoa mfano hatari kwa wanahabari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |