Rais Donald Trump wa Marekani amesema Marekani haina haja ya kuongeza askari kwenye eneo la Mashariki ya Kati, lakini atatuma askari bila ya kujali idadi yake wakati inapohitajika.
Wakati huo huo, kaimu waziri wa ulinzi na usalama wa Marekani Bw. Patrick Shanahan, amesema habari kuhusu mpango wa wizara yake wa kuongeza askari elfu 5 au elfu 10 huko Mashariki ya Kati si sahihi. Amesema Marekani itaongeza uwezo wa ulinzi wa kijeshi kwenye Mashariki ya Kati, kitendo ambacho kingehusiana na kuongezeka kwa kutuma jeshi lake. Amesisitiza kuwa lengo la Marekani ni kutishia siyo kuchochea vita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |