• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Messi atwaa kiatu cha dhahabu, Mbappe akikosa

    (GMT+08:00) 2019-05-27 09:15:36

    Mbio za kuwania kiatu cha dhahabu Ulaya hatimaye zimekamilila na rasmi Lionel Messi ameweka rekodi ya kuwa mtu wa kwanza kutwaa tuzo hiyo mara ya tatu mfululizo.

    Jambo hilo limetokana na Kylian Mbappe wa PSG kushindwa kuifikia idadi ya mabao 36 aliyofunga Messi katika La Liga msimu huu, akiishia na mabao 33.

    Mbappe ambaye ametisha kwa kiwango chake msimu huu akibeba tuzo ya mfungaji bora wa ligi kuu ya Ufaransa, alifunga goli moja ambalo halikutosha kuikoa PSG na kipigo cha ugenini dhidi ya timu hiyo inayoshika nafasi ya nane katika msimamo wa ligi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako